Monday, October 3, 2016

Pata kuijua historia ya Nyakijoga

b

30 October 2011

HIJA KWA BIKIRA MARIA NYAKIJOGA:Lurdi ya Bukoba yafanyika hii Leo 30-10-2011

HISTORIA FUPI YA NYAKIJOGA KWA UTAFITI a kituo cha Hija cha Parokia ya Mugana.
Wakati huo Parokia ya Mugana ilikuwa ikijiandaa kuadhimisha Jubilei ya Miaka 50 tangu ilipoanzishwa. Jubilei ilikuwa iadhimishwe mwaka 1955. Kituo hiki cha Hija kilianzishwa kwa madhumuni ya kushiriki kiroho katika maadhimisho ya Jubilei ya miaka 100 tangu tamko rasmi la Kanisa la mwaka 1854, kuwa ni nguzo ya imani kwamba Bikira Maria aliumbwa bila dhambi ya asili. Vilevile, mwaka 1958 kuliadhimishwa Jubilei ya miaka 100 tangu Bikira Maria mwenyewe alipomtokea msichana Bernadeta Subiru huko Lurdi Ufaransa mwaka 1858 na kujitambulisha kuwa yeye ndiyealiyeumbwa bila dhambi ya asili

Kwa kujitambulisha hivyo Bikira Maria athibitisha ukweli ambao ulikuwa unakubaliwa na Kanisa katika mapokeo yake ya kawaida (Tradition), ambao ulitamkwa rasmi na Kanisa mwaka 1854.

Ili kuwawezesha waumini wote wa Jimbo la Rutabo la nyakati zile kushiriki kikamilifu, Mwashamu Laureani Rugambwa, alimwomba Baba Mtakatifu Pio XII awaruhusu wote watakao Hiji hapa wapate rehema za Jubileo hiyo kuu ya Lurdi. Baba Mtakatifu aliruhusu. 

Mwasham Baba Askofu Nestory Timanywa wa Jimbo kuu la Bukoba akiongoza maandamano kuelekea Nyakijoga.Maandamano yameanzia katika kanisa kuu la Parokia ya Mugana.

Mapadre wakiwa kwenye Misitari.

Wahudumu wenye kubeba Sanamu ya Bikira Maria,pembeni ni Ndg Peter Mgisha mmoja wapo wa Mahujaji

Hija ni safari ya Imani afanyayo muumini kwenda mahala patakatifu kwa ajili ya sala,ibada na manufaa ya kiroho.Imani inaifanya safari ya hija iwe tofauti na na safari nyinginezo,kama vile utalii,mandari au matembezi tu.
Hija humfanya mtu abadili mwenendo wake wa maisha na kusogea karibu na na Mungu 

Wadau wakiwa kwenye Mistari kuelekea kwenye Maji ya Baraka wakati ibada ya Hija ikiendelea hii leo.

Mdau Mama Kasangwa akipata Maj ya Baraka.

Hivi ndivyo utitili wa magari ulivyo Mugana katika hija.

Wadau wa Pande za Muleba nao wamejitokeza kama unavyo mwona Ndg Geofle (katikati)

Camera yetu maeneo ya Mugana imenasa wadau hawa wakitelemka kwenye Fusso tena nyuma kwangu mie Mc kama blogger nimechukulia kama kituko.
Hili ndilo Jeshi letu la Polisi na haya ndio maisha waliomo.!!

Biashara kila aina ziliendelea

Mdau Godiliza,huyu jamaa wa Kitambo sana,Nimepata faraja kukutana naye uso kwa uso akiendeleza shughuli zake uko Mugana.

Swala la Hija Mugana linahistoria yake na umgusa kila mdau kwa namna anavyo elewa umuhimu,Pichani ni Mwana mama mjasilia mali akiendea na biashara yake.

Huduma ya Red cross waljipanga vyema.

Wakati likiingia gari la Jeshi likiwa limejaa wanakwaya wa Jeshi wakiwa wamevalia Sare zao kiasi ilinipendeza sana.

Wadau kutoka Pande Za Katoma Maarufu kama Mapacha,(kushoto) ni Mama Kazinduki

Mr Kyaruzi ,huyu pia ni mdau wa siku nyingi,kama unakumbuka au ulikuwepo enzi zile za Kaijanante Bondia maarufu basi huyu Kyaruzi ndiyo mpinzani wake,mfano wa Cheka na Maugo, na hiyo ndio faida ya Mimi kuwajua wadau wengi kwa %kubwa.

RMK ikiwa na abiria wa Kashai.

Walinzi wa Usalama katika hija.

Hivi ndivyo asa ilivyo kuwa Hija ya leo hii
Bukobawadau ndio katika kufatilia hili na lile pande zote hapa Mkoani.
Bukobawadau kufikia hapa hatuna la Ziada ,tunacho weza kusema ni kufanyia kazi na kutafakali Maneno yaliopo kwenye Gari hili mwisho wa Picha.

Tunatoa shukurani kwa kila Mdau anaye tembelea tovuti hii.

stevedaboy at 11:59 PM


 













2 comments: